July 20, 2013

Kazi za vijana wa Archtecture

 Kazi hii imeanza kujengwa






Karibu kwa ushauri elekezi Asante
Kwa mawasiliano zaidi 
boctor555@gmail.com/georgejohn1978@yahoo.com
simu +255 712371703/0757 836770/ 0767-551771

June 21, 2013

Kwa nini usiolewe eti....

Usiolewe eti kwa kuwa rafiki zako wengi wameolewa

Usiolewe kwa kuwa eti umemaliza chuo na una kazi nzuri

Usiolewe eti kwa kuwa mama na baba wanataka mjukuu

Usiolewe eti kwa kuwa marafiki zako wanataka kula Ubwabwa wa shughuli yako

Usiolewe kwa kuwa una gari zuri na maisha umeanza kuyapatia!

Usiolewe kwa kuwa wachungaji kanisani wanakuulizia eti na wewe unaoelewa lini?

Usiolewe kwa kuwa rafiki wa kiume wa kwanza kapita bila bila wapili, watatu, wanne wote kimya.... unaona kama umesahaulika...!

Usiolewe kwa kuwa umebeba mimba....ya huyo boyfriend wako ambaye uliyenaye....ilihali unaona kuwa hamtafika mbali....

Olewa baada ya Mungu kujibu maombi yako na kukupatia Mume mwema, utamjuaje ni mume mwema....?

Itaendelea toleo lingine....

By Mutasingwa 

June 14, 2013

Mahusiano na Mapenzi

Habari wanafamilia, leo naona nianze kusema nanyi kuhusu sula la Mahusiano na Mapenzi.

Ni kweli ukiwa na mpezi wako lazima mfanye ngono? ama ukimkatalia anasema nakupenda ila nitatafuta msichana mwingine ambaye ataniridhisha na kutimiza haja yangu ya kingono!

Maswaibu haya na mengine mengi yamekuwa ni mambo ambayo yanawaumiza hasa wasichana wengi... kuliko wavulana... eti msichana akipata mimba nani anaumia kati yake Msichana na Mvulana?

Bila shaka ni msichana, anaanza kuwaza sasa jamaa asiponioa nitakuwa mgeni wa nani? je wazazi wangu nitawaambia nini? na wakiniuliza mimba ya nani nitasemaje? kibaya zaidi urafiki wenu hamjauonesha kwa wazazi...

Kwa wasichana wanaumia sana na wavulana inakuwa ni kuonesha kwa masela kuwa yeye ni kidume/dume la mbegu... huu ni utoto wakati mwingine...kwani ukianzisha urafiki/mahusiano na msichana lazima muishie kufanya ngono? yapo mengi ambayo mnaweza kufanya mkiwa wote na kuridhishana kimahaba.....na kila mtu akalizika.... ila kwa hivi sasa suala hili linaoenekana ni gumu kwa vijana....

Vijana wengi wanakuwa na urafiki wa ushabiki na ukisha lala nae ama kufanya nae ngono ujue anaweza kukimbia!

Ushauri ni kuwa jitahidi kusubiri na kujiepusha na vitendo vya ngono ili mtimize ndoto zako..wakati mwingine unaweza kuwa na wasiwasi kuwa anaweza kunikimbia eti sijampa kile anataka! hasha, kama ipo ipo tu! Wahenga walisema kuwa "Wasiwasi nayo nia akili"

Ama mkishindwa kabisa tumia kondomu, ila mazungumzo yatawale hisia zenu

By Mutasingwa

June 07, 2013

UNYANYASAJI WA KIJINSIA

Unyanyasaji wa kijinsia, unachangia kwa kiasi kikubwa vifo kwa akina mama na watoto, maeneo ambayo vitendo hivi vimekithiri kwa Tanzania ni Mkoa wa Mara, wakati fulani nilikutana na Binti jina kapuni, alipigwa na mzazi wake kiasi kwamba ukiaangalia picha hizi utastaajabu kama kweli aliyetenda haya ni mzazi wa kumzaa.... sababu ya haya yote ni binti kuchelewa kurudi nyumbani akitokea matembezi ya sikukuu....ndipo mzazi alipoamua kumchapa fimbo akiwa amelala kifudifudi sehemu za mgongoni kwa zaidi ya saa mmoja.... hebu jiulize unyama na ukatili huu ulikuwa ni kiasi gani

 Ukiangalia picha hizi sio nzuri, ila kwa idhini ya mtedwa alisema kuwa zitumike ili jamii ione jinsi wazazi wanavyoweza kuwa zaidi ya binadamu wa kawaida....

Suala ambalo lilishangaza wakati wa mahojiano, mtoto alionesha kuridhika na kuonesha kuwa anamuachia Mungu haya yote..... Mie najiuliza ukatili huu mpaka lini?....

Hebu jamii na vijanakwa ujumla tufunguke na kusema hapana kwa ukatili wa aina hii

Labda tukumbushane haki zetu ambazo ni nadondoa kwa kiasi.....
1. Haki ya kuishi
2. Haki ya kulindwa
3.Haki ya kuheshimiwa na kutunziwa siri
4.Haki ya kupatiwa elimu
5. Haki ya kupatiwa huduma bora za afya
6. Haki ya kutoa maoni na kusikilizwa
7. Haki kucheza.....

Hapa kwa ufupi mzazi alikiuka haki ya kulindwa, na pengine kutishia pia haki ya Uhai kwa maana ya haki ya Kuishi. huyu alitakiwa kufikishwa mikononi mwa Dola na sheria kuchukua mkondo wake.....


By Mutasingwa

MATUMIZI YA KONDOM KWA VIJANA

Tangu ulipogunduliwa Ugonjwa wa UKIMWI, miaka ya 80s serikali ilianza jitihada za kupunguza maambukizi, ilianza suala la kuhamasisha vijana kubadili tabia, suala hili limeonekana kuwa gumu, kiasi kwamba tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa vijana wanaanza vitendo vya ngono wakiwa na miaka 10 hivi, kiasi kwamba kushindwa kujua hasa nini chanzo, harakati mbalimbali zimeendelea kwa wadau wote NGO, mashirika ya kidini na mengine kemkem,na wadau wa maendeleo bado jitihada zinaendelea maana vijana wanaonesha kutosikia la mkuu wala la Mhazini.... jambo hilo ndio linalo nisukuma kuona leo nijadilia kwa nini kondom kwa vijana. 

Zipo sababu kadhaa ambazo zinaashiria vijana kuanza vitendo vya ngono mapema

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na TACAIDS na NIMR wa 2011, mikoa ya Dodoma, na Mbeya umeonesha kuwa vitendo vya ngono vinaanza mapema kwa vijana wa kike na kiume, ripoti ya viashiria vya UKIMWI nchini kwa mwaka 2011/12 ya mwezi februari mwaka huu, imeonesha kuwa maambukizi ya UKIMWI kwa vijana kati ya miaka 15-19 na matokeo yake kuanza kujionesha miaka ya 23-24, aidha, maambukizi ya watoto wa kike ni asilimia 6.6 na kiume ni asilimia 2.8, kwa maana hiyo wasichana walau ni mara mbili ya watoto wa kiume.... hii ni hatari kwa ustawi wa jamii na upotevu wa nguvu kazi ya baadaye. Bado kondom haineshi kuimalika kwa watoto wa wa jinsi zote si kike au kiume!

Pili, masuala ya afya ya uzazi na ujinsia imeonekana ni miiko kuzungumwa katika jamii yetu, wakati tafiti zinaonesha kuwa endapo wazazi/walezi watazungumza masuala haya kwa uwazi, kunauwezekano wa kupunguza maambukizi ya UKIMWI kwa asilimia 0.9, je kipi bora?

Tatu suala la matumizi ya kondom, imeoneka ni msamiati kwa vijana.... hii inatokana na dhana potofu miongoni mwa vijana...eti kondom haina radha! eti ina baridi! eti ina vitundu vidogovidogo! eti inaweza kuzama wakati wa kujamiana.... je kipi bora? kuacha kabisa kutumia kondom kwa sababu ambazo hazipo kisayansi.... ama kutumia kujiepusha na madhara makubwa ya maambukizi ya VVU? hebu jitafakari na kuchukua hatua mapema kijana..

Aidha, muarobaini wa yote hayo ni kuanza elimu ya makuzi na malezi kwa watoto wakingali wadogo..kuanzia walau miaka 5 na kuendelea.... nini kifundishwe? itategemea kulingana na uelewa wa watoto... siku hizi utandawazi watoto wanaelewa sana sio kama enzi za MWAAALIM!

Wazazi na walezi wawalinde watoto na hatari ya kujiingiza katika ngono zembe na kuachana na Tamaa zisizo na msingi...jukumu la kuwalea watoto wako ni lako sio la mwingine...mkunje samaki akingali mbichi sio usubiri akauke itakuwa hatari...
ZINGATIA
A-cha kabisa ngono
B-akia na mwenzi mmoja
C-ondom ni muhimu ikibidi

By Mutasingwa   


May 11, 2013

...LABDA NADHAN UNGEPENDA KUJENGA KANISA....HEBU ANGALIA PICHA HIZI...

Pengine ungependa kujenga kanisa, kazi hizi pia zinafanyika na kwa Ubora ambao unautarajia

Pembeni Kulia

 Kulia sehemu ya Parking na ofisi
 Nyuma
Picha ya Kiwanja 
wasiliana nasi kwa namba ambazo utaziona hapo katika nyumba zilizotangulia

Karibu sana

UKIIPENDA NYUMBA HII WASILIANA NASI....

 Mbele
 Mbele kulia
 Picha ya juu
 
Nyingine hiyo.. simu zile zile kwa nyumba nilizoweka post zake ....
TIMIZA NDOTO YAKO YA KUMILIKI NYUMBA NZURI YA KISASA!
KARIBU SAAANA